Msanii Harmorapa ambaye sasa ana 'trend' na moja ya video ikimuonyesha
akicheza wimbo akiwa amevaa gauni amefunguka na kusema yeye hajavaa gauni la bosi
wake kama ambavyo watu wanadai bali yeye amevaa nguo ya kawaida katika video
hiyo.
Harmorapa amesema hayo katika kipindi cha eNewz na kudai kuwa yeye
alifanya 'cover' ya kitu alichofanya Alikiba kwa kuimba wimbo wa 'Brenda
Fassie' na kwa kuwa yeye anamkubali sana msanii huyo alivutiwa naye na ndiyo
maana aliamua kufanya na yeye.
"Unajua mimi namkubali sana Alikiba hivyo nilivyoona amefanya kitu
kile na mimi nikasema ngoja nifanye kama 'Cover' ila sikuvaa gauni la bosi
wangu wala sikuvaa gauni mimi naona niliva mavazi ya kawaida tu, labda nyinyi
ndiyo mnaona gauni lakini kwangu mimi ile ni nguo tu ya kawaida"
-Harmorapa.
0 comments :
Post a Comment